Pages

Subscribe:

Thursday, April 23, 2015

PICHA ZA MSHINDI WA TRACE MUSIC STAR KUTOKA TANZANIA

Bendera ya Tanzania imepeperushwa kwa mara nyingine tena kwenye jukwaa la muziki la kimataifa baada ya Mtanzania, Mayunga Malimi kushinda shindano la Airtel Trace Music Star lililo chini ya mtandao wa Airtel na kituo cha runinga cha Trace TV.

Mayunga akiimba kwa hisia kali kusherehekea ushindi wake
Mayunga akiimba kwa hisia kali kusherehekea ushindi wake

Fainali ya shindano hilo iliyodumu kwa masaa mawili, ilioneshwa Jumamosi iliyopita kupitia kituo cha runinga cha TRACE Urban ambapo washiriki wa nchi 13 walikuwa wakichuana.
Hongera Mayunga
Fainali ilifanyika jijini Nairobi, Kenya.
Mayunga alipewa ushindi na majaji akiwemo muimbaji wa Marekani kwenye asili ya Senegal, Akon, Devyne Stephens na muimbaji wa Ufaransa Lynnsha.

Akon akiwa na Mayunga baada ya kutangazwa mshindi
Mayunga baada ya kutangazwa mshindi

Mayunga aliwashinda wasanii wengi wawili walioingia kwenye hatua ya tatu bora ambao ni Jitey wa Nigeria na Baz kutoka Congo Brazzaville.

Mayunga akiwa haamini kama jina lake ndio limetajwa kama mshindi wa shindano hilo
Mayunga akiwa haamini kama jina lake ndio limetajwa kama mshindi wa shindano hilo

Mtanzania huyo aliupokea ushindi huo kwa furaha iliyopitiliza kiasi cha kupoteza fahamu kipindi alipotangazwa ushindi.

Mayunga akiwa amepoteza fahamu kwa muda
Mayunga akiwa amepoteza fahamu kwa muda

Kutokana na ushindi huo, Mayunga alishinda mkataba wa kurekodi muziki na label ya Universal Music wenye thamani ya $500,000 ambayo ni takriban shilingi milioni 900. Mayunga ni mtoto wa mwisho kwenye familia yao yenye makazi yao mjini Morogoro.
Tazama picha zaidi za fainali hizo na ushindi wa Mayunga.

Shangwe ilitawala baada ya mshindi kutangazwa
Shangwe ilitawala baada ya mshindi kutangazwa


Wasanii walimshawishi Mayunga kufanya muziki ni Chris Brown, Usher na Nuruelly
Wasanii walimshawishi Mayunga kufanya muziki ni Chris Brown, Usher na Nuruelly


Wimbo wa ushindi
Wimbo wa ushindi


Akon akimpa Mayunga maneno ya kumpa ujasiri
Akon akimpa Mayunga maneno ya kumpa ujasiri


Furahia kijana ni siku yako hii
Akon: Furahia kijana ni siku yako hii


Mayunga alipoteza fahamu mara baada ya kutangazwa mshindi
Mayunga alipoteza fahamu mara baada ya kutangazwa mshindi


Mayunga aliwahi kupitia Machozi Band inayomilikiwa na Lady Jaydee
Mayunga aliwahi kupitia Machozi Band inayomilikiwa na Lady Jaydee


Mayunga atakuwa chini ya usimamizi wa Universal Music ukiwa ni mkataba wa kurekodi na promotion wenye thamani ya dola laki tano
Mayunga atakuwa chini ya usimamizi wa Universal Music ukiwa ni mkataba wa kurekodi na promotion wenye thamani ya dola laki tano

RadekArtPhoto-5775
RadekArtPhoto-6102
RadekArtPhoto-6104
RadekArtPhoto-6114
RadekArtPhoto-6118
RadekArtPhoto-6234
RadekArtPhoto-6250
RadekArtPhoto-6255
RadekArtPhoto-6270
RadekArtPhoto-6334
RadekArtPhoto-6335
RadekArtPhoto-6336
RadekArtPhoto-6338
RadekArtPhoto-6340
RadekArtPhoto-6345

0 comments:

Post a Comment